Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki Monn anasema ana wai wasi mkuwa kufuatia kuendelea kwa mapigano nchini Sudan Kusini.
Kumeripitiwa mapigano nje na ndani ya mji wa Wau, kati ya wanajeshi ya serikalia na makundi yaliyojihami tangu Ijumaa.
Haijulikani wapiganaji hao ni akina nani.
Mashirika ya kutoa misaada yanasema kuwa maelfu ya raia wamekimbia na pia kuna ripoti za uporaji na vifo.
Hali
ni tete nchini Sudan Kusini licha ya kuundwa kwa serikali ya umoja,
yenye lengo la kumaliza vita vya wenyewe kwa wenyewe vilivyoanza mwaka
2013.
Mawaziri wa Leba kujiuzulu Uingereza
Image caption
Jeremy Corbyn
Hali ya wasiwasi
iliyoanzishwa na upigaji kura wa Uingereza kuondoka Jumuiya ya Ulaya
(EU) imekumba chama kikubwa cha upinzani cha Leba.
Nusu ya Baraza
la Mawaziri la upinzani linatarajiwa kujiuzulu hii leo likilalamikia
jinsi kiongozi wao Jeremy Corbyn alivyoongoza kampeni ya kura za maoni.
Wa
kwanza kuondoka alikuwa Waziri wa Afya, Heidi Alexander, aliyesema kuwa
Bwana Corbyn hana kipaji cha kushughulikia matatizo yanayokumba
Uingereza kwa wakati huu.
Awali, Waziri wa upinzani wa Mashauri ya
Kigeni, Hilary Benn, aliachishwa kazi kwa kile Bwana Corbyn alidai
kuwachochea wenzake waondoke katika baraza hilo iwapo Bwana Corbyn,
atakataa kuheshimu mswada wa kutokuwa na imani kwake.
Wafuasi wengi wa Leba walipiga kura kwa Uingereza kujiondoa katika Jumuiya ya Ulaya.
Belle 9 Feat. Izzo Bizness, Jux, G Nako, Mr Blue, Maua Sama - Burger Movie Selfie RMX (Official VIDEO)
Mr Blue Ft Alikiba - Mboga Saba (Video)
Breaking News: Orodha Ya Majina Ya Wanafunzi Waliochaguliwa Kujiunga Na Kidato Cha Tano Na Vyuo Vya Ufundi Kwa Mwaka 2016
OR-TAMISEMI inawatangazia majina ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na Kidato cha Tano na Vyuo vya Ufundi kwa mwaka 2016.
Wanafunzi
waliochaguliwa ni kutoka shule za Serikali na zisizo za Serikali. Jumla
ya wanafunzi 65,720 wakiwemo wasichana 29,457 na wavulana 36,263
wamechaguliwa kujiunga na Kidato cha Tano na Vyuo vya Ufundi.
Kati
ya wanafunzi waliochaguliwa 34,064 wakiwemo wasichana 13,466 na
wavulana 20,598 sawa na asilimia 52 watajiunga na masomo ya Sayansi na
Hisabati; na wanafunzi 30,897 wakiwemo wasichana 15,445 na wavulana
15,452 sawa na asilimia 47 wamechaguliwa kusoma masomo ya Sanaa na
Biashara na wanafunzi 759 wakiwemo wasichana 220 na wavulana 539 sawa na
asilimia 1 wamechaguliwa kujiunga na vyuo vya Ufundi.
Wanafunzi
waliochaguliwa kujiunga na Kidato cha Tano mwaka 2016 wataanza muhula wa
kwanza tarehe 11 Julai, 2016 na hakutakuwa na mabadiliko yoyote ya
shule.
Wanafunzi
wote wanatakiwa kuripoti katika shule walizopangwa kwa wakati. Endapo
mwanafunzi atachelewa kuripoti hadi tarehe 24 ambayo ndiyo siku ya
mwisho ya kuripoti, nafasi yake itachukuliwa na mwanafunzi mwingine
aliyekosa nafasi.
Imetolewa na Katibu Mkuu, OR-TAMISEMI
Tumia link hii kupata matokeo Waliochaguliwa kidato cha tano na vyuo vya ufundi 2016