Featured

Jumapili, 26 Juni 2016

Vita vyaendelea Sudan Kusini



Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki Monn anasema ana wai wasi mkuwa kufuatia kuendelea kwa mapigano nchini Sudan Kusini.
Kumeripitiwa mapigano nje na ndani ya mji wa Wau, kati ya wanajeshi ya serikalia na makundi yaliyojihami tangu Ijumaa.
Haijulikani wapiganaji hao ni akina nani.
Mashirika ya kutoa misaada yanasema kuwa maelfu ya raia wamekimbia na pia kuna ripoti za uporaji na vifo.
Hali ni tete nchini Sudan Kusini licha ya kuundwa kwa serikali ya umoja, yenye lengo la kumaliza vita vya wenyewe kwa wenyewe vilivyoanza mwaka 2013.

Mawaziri wa Leba kujiuzulu Uingereza


 
Image caption Jeremy Corbyn
Hali ya wasiwasi iliyoanzishwa na upigaji kura wa Uingereza kuondoka Jumuiya ya Ulaya (EU) imekumba chama kikubwa cha upinzani cha Leba.
Nusu ya Baraza la Mawaziri la upinzani linatarajiwa kujiuzulu hii leo likilalamikia jinsi kiongozi wao Jeremy Corbyn alivyoongoza kampeni ya kura za maoni.
Wa kwanza kuondoka alikuwa Waziri wa Afya, Heidi Alexander, aliyesema kuwa Bwana Corbyn hana kipaji cha kushughulikia matatizo yanayokumba Uingereza kwa wakati huu.
Awali, Waziri wa upinzani wa Mashauri ya Kigeni, Hilary Benn, aliachishwa kazi kwa kile Bwana Corbyn alidai kuwachochea wenzake waondoke katika baraza hilo iwapo Bwana Corbyn, atakataa kuheshimu mswada wa kutokuwa na imani kwake.
Wafuasi wengi wa Leba walipiga kura kwa Uingereza kujiondoa katika Jumuiya ya Ulaya.

Belle 9 Feat. Izzo Bizness, Jux, G Nako, Mr Blue, Maua Sama - Burger Movie Selfie RMX (Official VIDEO)

Mr Blue Ft Alikiba - Mboga Saba (Video)

Breaking News: Orodha Ya Majina Ya Wanafunzi Waliochaguliwa Kujiunga Na Kidato Cha Tano Na Vyuo Vya Ufundi Kwa Mwaka 2016


OR-TAMISEMI inawatangazia majina ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na Kidato cha Tano na Vyuo vya Ufundi kwa mwaka 2016. 

Wanafunzi waliochaguliwa ni kutoka shule za Serikali na zisizo za Serikali. Jumla ya wanafunzi 65,720 wakiwemo wasichana 29,457 na wavulana 36,263 wamechaguliwa kujiunga na Kidato cha Tano na Vyuo vya Ufundi. 

Kati ya wanafunzi waliochaguliwa 34,064 wakiwemo wasichana 13,466 na wavulana 20,598 sawa na asilimia 52 watajiunga na masomo ya Sayansi na Hisabati; na wanafunzi 30,897 wakiwemo wasichana 15,445 na wavulana 15,452 sawa na asilimia 47 wamechaguliwa kusoma masomo ya Sanaa na Biashara na wanafunzi 759 wakiwemo wasichana 220 na wavulana 539 sawa na asilimia 1 wamechaguliwa kujiunga na vyuo vya Ufundi.

Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na Kidato cha Tano mwaka 2016 wataanza muhula wa kwanza tarehe 11 Julai, 2016 na hakutakuwa na mabadiliko yoyote ya shule. 


Wanafunzi wote wanatakiwa kuripoti katika shule walizopangwa kwa wakati. Endapo mwanafunzi atachelewa kuripoti hadi tarehe 24 ambayo ndiyo siku ya mwisho ya kuripoti, nafasi yake itachukuliwa na mwanafunzi mwingine aliyekosa nafasi.

Imetolewa na Katibu Mkuu,
OR-TAMISEMI


Tumia link hii kupata matokeo Waliochaguliwa kidato cha tano na vyuo vya ufundi 2016

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumapili ya June 26




Copyright © 2015 TANZANIA YETU
| Distributed By Gooyaabi Templates