Featured

Jumanne, 3 Mei 2016

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumanne ya May 3


Afungwa kwa kuajili wafanyakazi wa darasa la saba



MKUU wa Chuo cha Uhasibu (IAA) Njiro mkoani Arusha, Profesa Johannes Monyo amehukumiwa kifungo cha nje kwa sharti la kutofanya kosa lolote ndani ya mwaka mmoja.

Hukumu hiyo ilitolewa Ijumaa iliyopita na Hakimu wa Mahakama ya Wilaya ya Arusha, Devotha Msofe baada ya kujiridhisha kuwa Profesa Monyo alifanya makosa ya kuajiri watumishi wanane wenye elimu ya darasa la saba bila kufuata misingi na kanuni za utumishi wa umma.

Hakimu Msofe alisema Profesa Monyo akiwa Mkuu wa Chuo cha Uhasibu Njiro, aliwaingiza watumishi wanane kwenye ajira ya kudumu bila ya kibali kutoka kwa Katibu Mkuu Kiongozi au Katibu Mkuu Utumishi.

Alisema kutokana na ushahidi uliotolewa mahakamani kwa mashahidi 10 pamoja na vielelezo vinane vilivyotolewa mahakamani hapo na upande wa mshtakiwa kuwa na mashahidi wawili, mahakama hiyo imejiridhisha pasipo shaka kuwa Profesa Monyo alifanya kosa hilo la kuajiri wafanyakazi hao wanane bila kufuata taratibu za kisheria.

“Mahakama imejiridhisha pasipo shaka kuwa ulifanya kosa hili la kuajiri wafanyakazi wanane bila kufuata misingi na kanuni za utumishi wa umma hivyo mahakama hii inakutia hatiani kwa kukupa kifungo cha nje kwa sharti la kuutofanya kosa lolote katika kipindi cha mwaka mmoja,”alisema Hakimu Msofe.

Awali, Mwanasheria kutoka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), Adam Kilongozi alidai kuwa Juni, 2010 Profesa Monyo anatuhumiwa kuwapa ajira watumishi wanane ambao ni Pamela Maboko, Samson Mbarya, Mawazo Ndaro, Juma Nyarutu, Lilian Ngowi, Godfrey Mollel, Musa Maiki na Salim Shabani.

Kosa jingine ni Profesa Monyo kwa kutumia mamlaka yake vibaya,kuwaingiza watumishi hao wanane katika ajira, ilhali akijua elimu zao ni darasa la saba. Hata hivyo, baada ya hukumu hiyo kutolewa, Profesa Monyo ameonesha kusudio la kukata rufaa kupitia kwa wakili wake, Severine Lawena.

Baada ya hukumu hiyo kutolewa, mwandishi  alimhoji Mwanasheria wa Takukuru, Kilongozi, kuhusu Sheria ya Utumishi wa Umma au Kanuni zake inasemaje juu ya mtumishi anapohukumiwa akiwa bado yupo kazini, ambapo alisema kama mtuhumiwa amehukumiwa na akaonesha nia ya kukata rufaa, basi hukumu hiyo inaweza kufanya kazi au kutofanya kazi hadi hapo rufaa itakaposikilizwa.

Alisisitiza kuwa Takukuru wameshatuma nakala hiyo ya hukumu Tume ya Utumishi wa Umma, mwajiri wa Profesa Monyo, ili mamlaka husika zilifanyie kazi suala hilo lakini pia ni lazima mwajiri wake naye ajiridhishe na hukumu hiyo.

Wafanyakazi wa Kiwanda cha Urafiki na Kampuni ya Vinywaji ya Pepsi (SBC) Wagoma.......Mabomu Yatumika Kuwatuliza, Polisi Apigwa Jiwe Kichwani



Miezi michache baada ya aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda kukwaruzana na Mbunge wa Ubungo (Chadema), Saed Kubenea chanzo kikiwa ni mgogoro wa Kiwanda cha Urafiki na kupelekana mahakamani, jana mabomu yalirindima kiwandani hapo wakati wafanyakazi wakiendeleza madai ya malimbikizo ya mishahara. 

Awali, viongozi hao walifikishana mahakamani baada ya Kubenea kudaiwa kumtukana Makonda ambaye kwa sasa ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam wakati wakitatua moja ya migomo ya wafanyakazi hao. 

Kubenea alihukumiwa kifungo cha miezi mitatu nje na kutotakiwa kutoa lugha ya matusi kama alivyofanya kwa mkuu huyo, lakini madai ya wafanyakazi wa Urafiki bado hayajapata suluhu. 

Katika vurugu hizo zilizoanza jana asubuhi askari mmoja alipigwa jiwe kichwani huku wafanyakazi watatu wakizirai. 

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Christopher Fuime alisema vurugu hizo zilianza baada ya wafanyakazi hao kutoelewana. 

“Waliokuwa tayari kuendelea na kazi walizuiwa na wenzao,” alisema Fuime. 

Akizungumzia kuhusu askari kupigwa jiwe baada ya kuwasili eneo la tukio huku wafanyakazi watatu wakizirai alisema: “Wamepelekwa hospitali na tunawashikilia watu wanne.”

Mgomo huo ulianza mwishoni mwa mwaka jana wakati wafanyakazi hao wakidai stahiki ya mishahara na posho za usafiri, chakula na pango la nyumba. 

Hukumu ya madai iliyotolewa Februari mwaka jana na Mahakama ya Kazi (CMA) iliagiza wafanyakazi hao zaidi ya 800 walipwe Sh4.5 bilioni kuanzia Aprili 30. 

Jana wakati wakifuatilia utekelezaji wa hukumu hiyo, vurugu zilitokea huku magari zaidi ya 10 yaliyosheheni askari yakiwasili eneo la kiwanda hicho na kufanikiwa kutuliza vurugu hizo. 

Meneja Rasilimali Watu wa kiwanda hicho, Dickson Machilika alisema uongozi upo tayari kuwalipa stahiki zao, lakini umepanga kulipa kwa awamu. 

Alisema uzalishaji wa kiwanda umeshuka na hata wafanyakazi wanaingia mara moja tofauti na awali kulipokuwa na awamu tatu. 

Wakati huohuo, Wafanyakazi wa Kampuni ya Vinywaji ya Pepsi (SBC) jana waligoma wakishinikiza uongozi wao kuwapa mikataba ya kuongezewa mishahara. 

Katika mgomo huo, polisi walilazimika kufyatua mabomu ya machozi kuwatawanya wafanyakazi hao ambao walikuwa mbele ya lango la kampuni hiyo wakiimba. 

Wafanyakazi hao waliilaumu kampuni hiyo kwa kumpa wakala jukumu la kuajiri na kulipa mishahara yao jambo linalosababisha ucheleweshwaji wa malipo. 

“Wakala hatumtaki na kwa nini kampuni kubwa kama hii badala ya kuajiri watu, wanawapa mawakala na kusababisha sisi kutolipwa haki zetu,” alisema Dunia Shabani.

Ofisa Uhusiano wa kampuni hiyo, Irenus Mushongi alisema anashangaa kitendo hicho kwani walifanya mazungumzo na wafanyakazi hao na walikuwa katika hatua za kutafuta ufumbuzi.

 “Mipangilio ipo tena kwa mujibu wa sheria nashangaa kabla ya makubaliano wamelianzisha,” alisema. 

Ofisa Kazi wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi na Ajira, Omari Sama alisema madai hayo yalifikishwa wizarani na kujadiliana na pande zote na kutoa muda kwa mwajiri kutekeleza madai yao ndani ya siku 30.

Mlinzi wa Wizara ya Ujenzi atupwa jela miaka mitatu Kwa Kosa la Kushindwa Kuzuia Wizi wa Kiti na Kompyuta


Mkazi wa Temeke Ramadhani Kusena (48) amehukumiwa kifungo cha miaka mitatu jela baada ya kupatikana na hatia ya kushindwa kuzuia wizi usitokee katika Wizara ya Ujenzi, wakati akiwa mlinzi wa eneo hilo. 

Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Wilaya ya Ilala, Catherine Kioja alisema jana kuwa mahakama imemtia hatiani mshtakiwa huyo baada ya kupitia ushahidi wa mashahidi wanne. 

Mbali na kifungo hicho, mahakama pia imemuamuru mshtakiwa huyo kulipa fidia ya Sh500,000 kwa kushindwa kuzuia wizi wa kiti na kompyuta katika chumba namba 303 kilichopo katika ofisi za wizara hiyo. 

Hakimu Kioja alisema mshtakiwa huyo anaweza kukata rufaa kama ataona hajatendewa haki na mahakama hiyo katika hukumu hiyo. 

Awali, kabla ya kutolewa kwa hukumu hiyo, upande wa mashtaka ukiongozwa na Wakili Grace Mwanga uliomba mahakama kutoa adhabu kulingana na shtaka hilo. Hata hivyo, Mahakama ilimpa nafasi mshtakiwa ajitete kwanini asipewe adhabu. 

Akijitetea, mshtakiwa huyo aliomba mahakama impunguzie adhabu kwa kuwa anategemewa na familia. Wakili Mwanga alisema mshtakiwa alitenda kosa hilo Julai 7, 2014 katika ofisi za wizara hiyo Mtaa wa Samora Dar es Salaam.

Kanisa Katoliki Lachomwa Moto Karagwe

Picha si ya tukio halisi

Watu wasiofahamika wamechoma moto Kanisa Katoliki Kigango cha Nyarwele, Parokia ya Kimiza, Jimbo la Kayanga wilayani Karagwe, Mkoa wa Kagera.

Katika tukio hilo la jana usiku, mali zote zilizokuwamo ndani ambazo thamani yake haijajulikana ziliteketea.

Shuhuda wa tukio hilo, Paulina Nkuba (67) alisema alifika eneo la tukio asubuhi baada ya kupewa taarifa na mjukuu wake anayesoma Shule ya Msingi Kimiza.

Alisema baada ya kufika katika eneo la tukio alipiga yowe kuomba msaada na alipoona watu hawatokei, alitoa taarifa kwa uongozi wa kitongoji ndipo waliwajulisha wananchi na kuanza kukusanyika. 

Paroko wa Parokia ya Kimiza, Padre Fortunatus Bijura alisema kitendo hicho ni cha kuhuzunisha na kusisitiza hawataacha kusali kwa kuwa hata chini ya mti watafanya ibada.

Askofu wa jimbo hilo, Almachius Vicent Rweyongeza aliwataka waumini wasilipize kisasi hata kama wakimjua aliyechoma kanisa hilo.

Mwenyekiti wa kamati ya kanisa hilo, Sabas Kafuba alivitaja baadhi ya vitu vilivyoteketea kuwa ni jengo, nyaraka, meza, viti, kinanda na jenereta.

Akizungumza na wananchi, ofisa upelelezi wa Wilaya ya Karagwe aliyejitambulisha kwa jina la Masoud aliwataka kuunda vikundi vya ulinzi na kutoa taarifa za kukomesha uhalifu huo.

Jumatatu, 2 Mei 2016

Jedwali la msimamo wa ligi ya EPL

Jedwali la msimamo wa ligi ya EPL kufikia 2 Mei, 2016.
NambariKlabuMechiMabaoAlama
1Leicester363077
2Tottenham353969
3Arsenal362567
4Man City363064
5Man Utd351260
6West Ham351759
7Southampton361457
8Liverpool351155
9Stoke36-1448
10Chelsea34747
11Everton35644
12Watford35-644
13Swansea36-1343
14West Brom36-1441
15Bournemouth36-2041
16Crystal Palace36-1039
17Newcastle36-2533
18Sunderland35-1832
19Norwich35-2631
20Aston Villa36-4516

Leicester City kunyemelea ushindi Epl?

Image copyrightbbc
Image captionLeicester City imetoka sare ya 1-1 ilipokutana na Manchester United
Leicester City wamebakiwa na alama mbili pekee kuupata ushindi wa ligi kuu ya England baada ya kupata sare ya 1-1 dhidi ya klabu ya Manchester United katika dimba la Old Trafford huku wakitegemea matokeo ya mchezo kati ya Chelsea dhidi ya Tottenham utakaopigwa leo hii majira ya saa nne usiku kwa saa za afrika mashariki katika dimba la Stamford Bridge.
Mbweha walipata afueni baada ya kuwa nyuma kwa goli moja lililofungwa na Antony Martial dakika ya nane ya mchezo kabla ya kusawazisha na kepten Wes Morgan dakika ya 17. Pande zote mbili zilinyimwa mikwaju ya penalti baada ya mlinzi Marcos Rojo kumzuia Riyad Mahrez ndani ya eneo la 18 huku pia Danny Drinkwater wa Leicester akimvuta Memphis Depay ndani ya eneo la hatari.
kwa matokeo hayo Leicester wanaendelea kubaki kileleni mwa ligi ya England wakiwa na alama 77. Claudio Ranieri huyo akisisitiza kuwa hawakufuata kikombe OT bali kucheza mchezo safi lakini Man U walikua wazuri zaidi yao. Matokeo mengine Liverpool walikiona cha mtema kuni baada ya kuchapwa 3-1 walipokuwa wageni wa Swansea huku Man city wakiambulia kichapo cha mbwa mwizi 4-2 walipowatembelea Sauthampton

Wenger: Nilitarajia mabango zaidi Emirates

WengerImage copyrightAFP
Image captionWenger anasema mashabiki wana haki ya kulalamika
Meneja wa Arsenal Arsene Wenger amesema alitarajia mashabiki zaidi waonyeshe kutoridhishwa naye wakati wa mechi ya Jumamosi dhidi ya Norwich.
Arsenal walishinda 1-0.
Wenger atatimiza 20 kwenye usukani Arsenal Oktoba mwaka huu lakini mara yake ya mwisho kushinda ligi ilikuwa 2004 na baadhi ya mashabiki waliinua mabako ya kusema “wakati wa mabadiliko umefika” uwanjani Emirates.
"Nilidhani uwanja wote ungegeuka na kuwa wa rangi nyeupe (kutokana na mabango),” amesema.
"Lengo letu kuu ni kuwafanya watu wote 100% wafurahi. Kwa bahati mbaya, hatukuweza kufanya hilo msimu huu.”
Ushindi wa Jumamosi uliwawezesha Arsenal kuwapita Manchester City, ambao watakuwa wenyeji wa The Gunners uwanjani Etihad Jumamosi, na kutua nambari tatu jedwali la Ligi ya Premia.
Arsenal wanahitaji alama mbili kutoka kwa mechi zao zilizosalia kujihakikishia nafari katika Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya msimu ujao, kwa mara ya 18 mtawalia.
ArsenalImage copyrightAll Sport
Image captionBaadhi ya mashabiki hawajafurahia kushindwa kwa Arsenal kushinda ligi
Wakati wa mechi hiyo ya Norwich, baadhi ya mashabiki walinyanyua mabango dakika za 12 na 78 za mechi, kuachilia miaka 12 tangu Arsenal walipotawazwa mabingwa ligi mara ya mwisho.
Lakini kunao wengine walioeleza uungaji mkono wao kwa Wenger.
"Mimi ni mtu wa soka. Mimi si mwanasiasa,” alisema Wenger, 66.
"Simo katika mfumo wa demkrasia. Nitakuwepo mechi ijayo, kusimamia mechi, kujaribu kufanya vyema na nakubali maoni ya watu,” alisema.
Mkataba wa Wenger utamalizika msimu wa 2016/17 na anasema hapangi kung’atuka kabla ya wakati huo.
Copyright © 2015 TANZANIA YETU
| Distributed By Gooyaabi Templates